Jumatatu 24 Agosti 2026 - 23:42
Mashambulizi ya Kikatili ya Utawala wa Kizayuni Dhidi ya Lebanon Yaendelea

Hawzah/ Adui wa Kizayuni ameendelea na mashambulizi yake dhidi ya kusini mwa Lebanon na kukiuka mamlaka na uhuru wa nchi hiyo, kupitia mashambulizi ya anga, operesheni za kulipua na kuchoma moto nyumba, pamoja na mashambulizi ya mabomu ya mizinga dhidi ya vijiji.

Kwa mujibu wa ripoti ya Kitengo cha tarjama cha Shirika la Habari la Hawza, adui wa Kizayuni ameendelea na uvamizi wake dhidi ya kusini mwa Lebanon na kukiuka mamlaka na uhuru wa nchi hiyo kupitia mashambulizi ya anga, operesheni za milipuko na uchomaji wa nyumba, pamoja na mashambulizi ya mabomu ya mizinga dhidi ya vijiji.

Jeshi la adui lilichoma moto nyumba kadhaa katika kijiji cha Zouter al-Sharqiyah, na kutekeleza operesheni za milipuko katika maeneo ya malisho ya kijiji cha Al-Mansouri, upande wa Majdal Zoun. Aidha, adui wa Israel alifanya mashambulizi katika kijiji cha Zouter al-Sharqiyah.

Ndege za kivita za utawala wa Kizayuni zilishambulia kwa mabomu maeneo ya Ali al-Taher, Doha Kafr Rumman na Al-Nabatieh Al-Fawqa. Wakati huo huo, adui alilenga kwa mabomu ya mizinga kijiji cha Mais al-Jabal na maeneo ya jirani, na kulipua kwa mabomu eneo lililopo kati ya vijiji vya Beit Yahoun na Baraachit. Maeneo ya Ali al-Taher na Al-Dabshah, pamoja na vijiji vya Al-Qantara, Al-Mansouri na Doha Kafr Rumman, pia yalilengwa na mashambulizi ya mabomu ya mizinga; huku mizinga ya adui ikilenga maeneo ya Ali al-Taher na Doha Kafr Rumman kwa mabomu ya fosforasi yaliyopigwa marufuku kimataifa.

Ndege ndogo isiyo na rubani ya adui wa Kizayuni ilidondosha bomu katika eneo lililopo kati ya vijiji vya Al-Haniyah na Al-Qulaylah, huku ndege nyingine ndogo ya adui ikidondosha bomu la sauti juu ya tingatinga katika kijiji cha Yater, ambalo halikusababisha hasara yoyote.

Katika hali hiyo hiyo, ndege zisizo na rubani za adui wa Israel zimeendelea kukiuka anga ya Lebanon, na hadi wakati wa kuandaliwa kwa ripoti hii, safari za ndege hizo zilikuwa zikiendelea juu ya anga ya Dhahiyah ya Kusini mwa Beirut, mji mkuu wa Lebanon.

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha